Mh. Samuel Sitta ataongoza msafara na mazishi ya marehemu Ramadhani Fundikira mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege mjini Tabora mnamo saa 5:30 asubuhi na taratibu nyingine zitaendelea kama kawaida. Katika msafara huo Mh. Sitta ataongozana na watu wengi akiwemo Mh. Aden Rage mb. wa Tabora mjini wakiongozana na watoto wa marehemu; Saidi, Adam, Chelu, Nzwala na Mkala mpwa wa marehemu


Mzee Ramadhani Fundikira wakati wa uhai wake, (1927-2014). Alifariki tarehe 03/04/2014 saa 10:30 alfajiri katika hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni , Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na figo kwa takriban wiki 3.
Mwili unatarajiwa kusafirishwa kesho Tarehe 5/4/2014 na kuzikwa kijijini kwao Itetemia, Tabora, huku muda unakadiriwa kuwa ni saa 7 mchana.
TARIFA ZOTE MUHIMU ZITAWAJIA KUPITIA MTANDAO HUU.
TUNAUNGANA NA FAMILIA NZIMA KIPINDI CHOTE KIGUMU CHA MAOMBOLEZO YA MPENDWA WETU
Mwili unatarajiwa kusafirishwa kesho Tarehe 5/4/2014 na kuzikwa kijijini kwao Itetemia, Tabora, huku muda unakadiriwa kuwa ni saa 7 mchana.
TARIFA ZOTE MUHIMU ZITAWAJIA KUPITIA MTANDAO HUU.
TUNAUNGANA NA FAMILIA NZIMA KIPINDI CHOTE KIGUMU CHA MAOMBOLEZO YA MPENDWA WETU






