
Taarifa zilizotufikia hivi punde zimedai kuwa rapper Geez Mabovu amefariki dunia leo mjini Iringa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Iringa, Geez amefariki jioni hii. Alienda kwao wiki moja na nusu iliyopita ambako alianza kuugua mfululizo. Taarifa zaidi zinakuja.
December 27 mwaka jana, hitmaker huyo wa Mtoto wa Kiume alizidiwa ghafla kabla ya show iliyokuwa ifanyike mjini Iringa kwenye ukumbi wa Twista Night Club alikokuwa atumbuiza na rappers wengine wakiwemo Wakazi, Songa, Jan B na Chidi Benz.
Source: Bongo5
Pia mtandao wa matukiodaima.co.tz uliandika;
"Mwanamuziki wa kizazi kipya Ahmed Ally Upete a.k.a G mabovu amefariki majira ya saa mbili usiku Iringa. Leo tarehe 12/11/14








