Pichani juu ni baadhi ya Watu wakitazama ajali iliyotokea maeneo ya Hedaru Wilayani Same mkoani Kilimanjaro Jumapili jioni ya tarehe 12/10/2014, ambapo ajali hiyo ilihusisha gari ndogo yenye namba za usajili T653 BZR kuingia chini ya uvungu wa basi la abairia lijulikanalo kwa jina la Happy Nation, kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa abiria wote waliokuwemo ndani ya gari ndogo (ambao idadi yao haikujulikana) walipoteza maisha papo hapo. Aidha bado haikufahamika mapema chanzo cha ajali hiyo ni nini.
Mmojawapo aliyetambulika kwa jina la Dennis (Enzi za Uhai wake) inasemekana alikuwemo katika gari ndogo na alipoteza maisha palepale.
MUNGU AZILAZE ROHO ZA MAREHEMU PAHALA PEMA PEPONI.
















